Monday, February 11, 2013

VURUGU ZA KIDINI GEITA

 
Majeruhi Sadick Yahya

Polisi na raiya

majeruh Said Ntahompagaze aliyejeruiwa mguu

Polisi na raiya
Imeripotiwa katika mitandao mbali mbali kuwa leo zimetokea vurugu za kidini nchini kati ya Waislam na Wakristu, katika kijiji cha Buselesele Wilayani Chato Mkoani Geita na kupelekea watu 10 kujeruhiwa vibaya huku mchungaji wa kanisa la Pentekoste Assemblies of God Mathayo Kachila (45) akipoteza maisha chanzo cha vurugu hizo kikiwa ni mvutano katika uchinjaji wa wanyama kwa ajili ya kitoweo. 

Mbali na mchungaji huyo kupoteza maisha, wengine waliojeruhiwa ni pamoja na Said Ntahompagaze(45), Sadick Yahaya(40), Yasin Rajab(56), Vicent Damon(22), wote wakazi wa Buselesele na mtu mmoja aliyefahamika kwa jina moja la Ramadhani ambaye yuko mahututi katika wodi namba nane katika hospital ya wilaya ya Geita.

Kwa sasa Waislam ndio wanaotambulika kuwa na dhamana ya kuchinja katika mchinjio ya serikali.

No comments: