Monday, December 19, 2016

UMUHIMU WA KUCHUNGA WAKATI



Makala hii muhimu itagusia sana umuhimu wa Muislamu kuchunga muda wake na kutokuuangamiza kwa kufanya mambo ya kipuuzi ambayo hayatomsaidia si duniani wala Akhera. Waislamu wengi tunashinda siku kutwa na kujishughulisha na mambo ya kipuuzi ambayo mengi katika hayo hayamridhishi Allaah.
Kwanza kabla ya kuendelea tungelipenda kurudi nyuma kidogo tukumbushane lengo la sisi kuwa hapa duniani ni lipi, kwa nini MwenyeZimungu ametuumba. Allaah anasema katika Qur-aan:

”Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi”

Thursday, April 28, 2016

TABIA NJEMA


Sifa njema zote Anastahiki Allaah Mola wa viumbe wote na rehma na amani zimfikie Mtume wetu Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), Jamaa na Swahaba zake wote.
Hivi unajua ndugu yangu Muislam, Allaah Akulinde na Akuhifadhi, kwamba 'amali iliyo bora zaidi na inayopendwa na Allaah Mtukufu na Mtume wake ni tabia njema?
Katika Hadiyth sahihi: Kutoka kwa Sa'ad bin Abiy Waqqaas (Radhiya Allaahu 'anhu) amesema Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Hakika Allaah Anapenda tabia njema na Anachukia tabia mbaya"