Sunday, November 3, 2013

MATOKEO YA DARASA LA SABA 2013, HAYA HAPA

 
 
Matokeo ya Darasa la Saba yametangazwa jana na mwaka huu ufaulu umeongezeka kutoka asilimia 30.72 mwaka jana mbaka asilimia 50.61 mwaka huu kutokana na wanafunzi walio fanya mtihani mwaka huu wa darasa la saba kufaulu zaidi ukilinganisha na wanafunzi wa mwaka jana.
Kaimu mtendaji wa Baraza la Mtihani Charles Msonda amesema ufaulu katika masomo yote umepanda kwa asilimia kati ya 6.01 na 28.06 ukilinganisha na mwaka 2012 Mwaka huu watahiniwa wamefaulu zaidi katika somo la Kiswahili kwa asilimia 69.06 na somo walio faulu kwa kiwango kidogo zaidi ni somo la Hisabati wamefaulu kwa asilimia 28.62, Msonda amesema jumla ya watahiniwa 427,606 kati ya 844,938 walio fanya mtihani huo wamepata alama ya 100 kati ya alama ya 250 idadi hiyo ni sawa na asilimia 50.61.
 

Saturday, November 2, 2013

Du’aa Ya Malaika Kila Siku Kwa Mtoaji Sadaka Na Mzuiaji

 عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه)  أَنَّ النَّبِيَّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((مَا مِنْ يَوْمٍ يُصْبِحُ الْعِبَادُ فِيهِ إلاَّ مَلَكَانِ يَنْزِلاَنِ فَيَقُولُ أَحَدُهُمَا: اللَّهُمَّ أَعْطِ مُنْفِقًا خَلَفًا. وَيَقُولُ الأَخَرُ: اللَّهُمَّ أَعْطِ مُمْسِكًا تَلَفًا)) متفق عليه
Imepokelewa kutoka kwa Abu Hurayrah(رضي الله عنه)  kwamba Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Kila siku inayowapambaukia watu kuna Malaika wawili wanateremka, mmoja wao akiomba: Ee Allaah! Mwenye kutoa [sadaka] mlipe zaidi. Na mwengine huomba: Ee Allaah! Mwenye kuzuia mpe hasara)).[1]

Sunday, October 27, 2013

Mwanamke Asifunge Swawm Au Kumuingiza Mtu Kwenye Nyumba Bila Ya Idhini Ya Mumewe

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه)  أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((لاَ يَحِلُّ لِلْمَرْأَةِ أَنْ تَصُومَ وَزَوْجُهَا شَاهِدٌ إلاَّ بِإِذْنِهِ. وَلاَ تَأْذَنَ فِي بَيْتِهِ إلاَّ بِإِذْنِهِ)) متفق عليه وهذا لفظ البخاري
Imepokelewa kutoka kwa Abu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Mtume wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Si halali kwa mwanamke kufunga Swawm [ya Sunnah] ilhali mumewe yupo [hakusafiri] ila kwa idhini yake. Wala asimruhusu mtu kuingia nyumbani kwake ila kwa idhini yake)).[1]
 

Tuesday, October 22, 2013

Nimemdanganya Mume Wangu, Je, Nimeachika? Na Je, Inanipasa Nikae Eda


SWALI:
Bibi na Bwana wameelewana kutumia koil kukinga kupata mtoto kwa mda. Kisha bwana ameamua koil bibi akaitowe. Bibi akamwambia bwana haya. Ikapita mdaa. Bwana akamuuliza bibi kama ile koil ameitoa? Bibi akadaganya mumewe kwamba koil kesha itowa. Baadae siku kadha bwana akamwambia bibi nafikiri kua koil hujaitoa umenidaganya. Na kama umenidaganya jua nishakuwacha. Bibi ana watoto watatu. WA miaka mitatu, na miwili na mmoja. Kazi ya ulezi pekee yake. Sababu bwana anafanya kazi kuazia jumatatu hadi ijumaa.   Swala langu ni, jee huyu mwanake kishawachika? Swala la pili kwa kua anahakika kua anatumia koil kutokupata mimba jee. Jee akiachika anakaa edaa? Insha’Allah nitapata majibu ya kuniridhisha. Asalaam aleikum.

Wednesday, August 21, 2013

NAFASI ZA KAZI KATIKA TAASISI YA UTAFITI WA MIFUGO (TALIRI) NALIENDELE - MTWARA


THE UNITED REPULIC OF TANZANIA
MINISTRY OF LIVESTOCK AND FISHERIES DEVELOPMENT

Telegrams: Scientific Mtwara                                   Tanzania Livestock Research Institute
Tel: +255 073 293 4035                                         Naliendele
Fax: +255 073 293 41                                            P. O. Box 509
Email: utafiti@iwayafrica.com                                  MTWARA
            In reply please quote:
            Kumb Na. MLD/NAL/F/2/Vol. 1/38

KWA YEYOTE ANYEHUSIKA:

YAH: NAFASI ZA KAZI KATIKA TAASISI YA UTAFITI WA MIFUGO (TALIRI) NALIENDELE-MTWARA

Tafadhali rejeeni kichwa cha habari hapo juu.

Napenda kuwatangazia kuwa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) iliyoanzishwa kwa Sheria Namba 4. Ya mwaka 2012 ya bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inazo nafasi za kazi kwa wale watakaopenda kufanya kazi katika Taasisi ua Utafiti wa Mifugo Naliendele-Mtwara. Nafasi zilizopo kwa sasa ni kama ifuatavyo:

Wednesday, August 7, 2013

MAMBO MATATU YANAYOFUATIA RAMADHAN


Zakaatul-Fitwr, 'Iydul-Fitwr Na Swawm Ya Sittatush Shawwaal

Tunakaribia kumaliza mwezi Mtukufu wa Ramadhaan na mambo matatu yafuatayo ya muhimu yanayotukabili yanapasa kuzingatiwa ili tukamilishe Swawm zetu ipasavyo na tupate fadhila zake.

1- ZAKAATUL-FITWR  
Inaitwa Zakaatul-Fitwr (Zakaah ya Kufuturu au Kufutari) kutokana na kumalizika Swawm ya Ramadhaan. Imefaridhiwa mwaka wa pili wa Hijrah katika mwezi wa Ramadhaan. 
Hikmah Yake
Ni kutwaharisha Swawm ya Muislamu kutokana na maneno machafu, ya upuuzi wakati alipokuwa amefunga kwa kulisha maskini chakula ili nao wapate chakula kizuri siku ya ‘Iyd.

Friday, August 2, 2013

ZAKAATUL FITWR


Zakaah Apewe Nani? 
SWALI
Zakaatul-Fitwr apewe nani? Je, inaruhusiwa kuituma mfano kwa Mujaahidiyn waliko vitani? Au kuitoa katika vyama vinavyokusanya sadaka au kujengea msikiti?

JIBU:
Sifa zote ni za Allaah.
Zakaatul-Fitwr inapaswa kupewa maskini Waislamu katika nchi au mji ambao inatolewa kwa sababu ya usimulizi wa Abu Daawuud kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhiya Allaahu 'anhuma) ambaye amesema: "Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ameamrisha Zakaatul-Fitwr ilipwe Ramadhaan kuwalisha watu masikini…."

Inaruhusiwa kuituma kwa masikini wa nchi nyingine ambao watu wake wanahitaji zaidi. Hairuhusiwi kujengea msikiti au kuitoa katika miradi ya sadaka.
Halmashauri ya Kudumu ya Utafiti Wa Kiislaam na utoaji wa Fatwa.

Tuesday, July 30, 2013

MASIKU YA KUMI LA MWISHO LA MWEZI WA RAMADHAN


Masiku ya kumi la mwisho la mwezi mtukufu wa Ramadhani, yana fadhila na khususia nyingi kathiri, miongoni mwake ni pamoja na kwamba:
i. Ndani ya masiku hayo umo usiku wa cheo/heshima, ambao huo ni bora kuliko miezi alfu moja. Na ye yote atakaye simama kufanya ibada katika usiku huo, kwa kumuamini Allah kikweli na kwa kutaraji ujira kutoka kwake, huyo atasamehewa dhambi alizokwisha zitenda.

Saturday, July 6, 2013

MWEZI WA RAMADHAAN IMETEREMSHWA QUR-AAN - JICHUMIE FADHILA ZA KUSOMA NA KUHIFADHI QUR-AAN

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala)  
(( شَهْرُ رَمَضَانَ الَّذِيَ أُنزِلَ فِيهِ الْقُرْآنُ هُدًى لِّلنَّاسِ وَبَيِّنَاتٍ مِّنَ الْهُدَى وَالْفُرْقَانِ))

((Mwezi wa Ramadhaan ambao imeteremshwa humo Qur-aan kuwa ni uongofu kwa watu, na hoja zilizo wazi za uongofu na upambanuzi)) [Al-Baqarah: 184]
Kwa hivyo basi ndugu Muislamu, jitahidi ufanye ibada hii adhimu usome na kuhifadhi Qur-aan kwa wingi kabisa kwani thawabu na fadhila zake ni nyingi na adhimu mno kama tunavyozinukuu humu. Pia jitahidi uweze kuhitimisha (kumaliza kuisoma) japo mara moja Qur-aan nzima kabla ya mwezi wa Ramadhaan kwisha.

Tuesday, June 25, 2013

NJIA10 ZA KUUKARIBISHA VIZURI MWEZI WA RAMADHAN

Anasema Allaah سبحانه وتعالى:

((يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُواْ كُتِبَ عَلَيْكُمُ الصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ)) (( أَيَّامًا مَّعْدُودَاتٍ فَمَن كَانَ مِنكُم مَّرِيضًا أَوْ عَلَى سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ وَعَلَى الَّذِينَ يُطِيقُونَهُ فِدْيَةٌ طَعَامُ مِسْكِينٍ فَمَن تَطَوَّعَ خَيْرًا فَهُوَ خَيْرٌ لَّهُ وَأَن تَصُومُواْ خَيْرٌ لَّكُمْ إِن كُنتُمْ تَعْلَمُونَ))  ((شَهْرُ رَمَضَانَ الَّذِيَ أُنزِلَ فِيهِ الْقُرْآنُ هُدًى لِّلنَّاسِ وَبَيِّنَاتٍ مِّنَ الْهُدَى وَالْفُرْقَانِ فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ وَمَن كَانَ مَرِيضًا أَوْ عَلَى سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ يُرِيدُ اللّهُ بِكُمُ الْيُسْرَ وَلاَ يُرِيدُ بِكُمُ الْعُسْرَ وَلِتُكْمِلُواْ الْعِدَّةَ  وَلِتُكَبِّرُواْ اللّهَ عَلَى مَا هَدَاكُمْ  وَلَعَلَّكُمْ  تَشْكُرُونَ))  
((Enyi mlioamini! Mmefaradhishiwa Swawm, kama waliyofaradhishiwa waliokuwa kabla yenu ili mpate kumcha Allaah))(([Mfunge] siku maalumu za kuhisabika. Na atakayekuwa miongoni mwenu mgonjwa au yumo safarini basi atimize hisabu katika siku nyengine. Na wale wasioweza, watoe fidiya kwa kumlisha masikini. Na atakayefanya wema kwa kujitolea, basi ni bora kwake. Na mkifunga ni bora kwenu, kama mnajua))  ((Mwezi wa Ramadhaan ambao imeteremshwa humo Qur-aan kuwa ni uongofu kwa watu, na hoja zilizo wazi za uongofu na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini katika mwezi huu na afunge. Na mwenye kuwa mgonjwa au safarini, basi atimize hisabu katika siku nyengine. Allaah Anakutakieni yaliyo mepesi wala Hakutakieni yaliyo mazito, na mtimize hiyo hisabu, na mumtukuze Allaah  kwa kuwa Amekuongoeni ili mpate kushukuru)) [Al-Baqarah: 183-185]

Friday, May 10, 2013

TANGAZO KUHUSU NAFASI ZA MAFUNZO YA KILIMO NGAZI YA CHETI NA DIPLOMA KWA MWAKA WA MASOMO 2013/2014



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA KILIMO CHAKULA NA USHIRIKA



TANGAZO KUHUSU NAFASI ZA MAFUNZO YA KILIMO NGAZI YA CHETI NA DIPLOMA KWA MWAKA WA MASOMO 2013/2014
Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika inatangaza nafasi za mafunzo ya Kilimo ngazi ya Cheti na Diploma kwa mwaka wa masomo 2013/14 kama ifuatavyo:

Wednesday, May 1, 2013

HOTUBA YA MH. JAKAYA MRISHO KIKWETE KATIKA SHEREHE YA MAADHIMISHO YA SIKU YA WAFANYAKAZI DUNIANI



Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Nchini (TUCTA),
Ndugu Ayoub Omari Juma;
Mheshimiwa Jaji Mkuu;
Mheshimiwa Gaudensia Kabaka (Mb) Waziri wa Kazi na Ajira;
Mhe. Col Issa Machibya, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro;
Waheshimiwa Mawaziri na Wabunge Mliopo Hapa;
Ndugu Alexio Musindo, Mwakilishi wa Shirika la Kazi Duniani (ILO)


Wednesday, April 17, 2013

NGUZO ZA SWALA, VITENDO VYA WAAJIB NA SUNNAH KATIKA SWALA


بسم الله الرحمن الرحيم


Nguzo za Swalah ni 14: Nguzo ni zile ambazo ukiswali na ukaziacha kwa makusudi Swalah yako inabatilika, na ikiwa umeacha kwa kusahau, Swalah yako pia itakuwa haikukamilika hadi urejee kitendo chenyewe au urejee rakaa na kisha mwishoni utoe Sajdatus-Sahw. Lakini ukiwa umesahau nguzo ya Takbiyratul-Ihraam, basi itakubidi uiswali Swalah upya tokea mwanzo.

Saturday, April 13, 2013

WALIOCHOMA MSIKITI TUNDUMA BADO HAWAJAFIKISHWA MAHAKAMANI



Waliochoma msikiti Tunduma bado hawajafikishwa mahakamani. Habari kutoka katika mji huo mdogo katika Mkoa wa Mbeya zinafahamisha kuwa Jeshi la Polisi, linaendelea kuwashikilia watuhumiwa 45 wa vurugu za kuchinja na kuchoma moto Msikiti. Awali Jeshi la Polisi l i l i w a t i a m b a r o n i watuhumiwa wa vurugu na maandamano hayo wapatao 90 na baada ya mahojiano, wamechujwa na kubakia 45. 

Wednesday, April 10, 2013

KUMUANDAA MNYAMA KABLA YA KUCHINJWA - STUNNING




Hii ni njia inayotumika kumuandaa mnyama kabla ya kuchinjwa, nia kuu ya stuning ni kumpunguzia mnyama maumivu wakati wa kuchinjwa, pia huondoa uwezekano wa mnyama kumuumiza mchinjaji na mwisho ni kuongeza ubora wa nyama.

Saturday, April 6, 2013

Watuhumiwa Kesi ya Sheikh Ponda‘wawakaanga’ Polisi mahakamani

 
 
Gazeti la ANNUUR Na. 1061
RABBIUL THAN 1434,
IJUMAA MACHI 8 - 14, 2013
Na Bakari Mwakangwale

Watuhumiwa Kesi ya Sheikh Ponda‘wawakaanga’ Polisi mahakamani

Wadai walivamiwa msikitini wakiwa katika ibada.
Waikana BAKWATA na kudai hawazijui kazi zake.
Wasema kiongozi wao ni Qur’an na Sunna za Mtume

MASHAHIDI wa upandewa utetezi katika kesi inayomkabili Sheikh Ponda Issa Ponda, wamedai askari Polisi waliwavamia na kuwapiga wakiwa katika ibada ya Itiqafu, ndani ya Msikiti wa MarkazChang’ombe, jijini Dar esSalaam, usiku wa Oktoba16, 2012.

Tuesday, April 2, 2013

HOTUBA YA MHE. JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, KWA WANANCHI, TAREHE 31 MACHI, 2013





 Rais Jakaya Mrisho Kikwete


Ndugu Wananchi;
Naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujaalia uhai na kunipa fursa ya kuzungumza nanyi kwa kupitia utaratibu wetu huu mzuri wa kila mwisho wa mwezi.  Leo ninayo mambo matatu ninayopenda kuzungumza nanyi.

Tuesday, February 26, 2013

TAMKO LA JUMUIYA NA TAASISI ZA KIISLAM - MAUAJI YA PADRI



TAMKO LA JUMUIYA NA TAASISI ZA KIISLAMU ZANZIBAR KULAANI MASHAMBULIZI NA MAUAJI YA VIONGOZI WA DINI PAMOJA NA KUPINGA KAULI ZA UCHOCHEZI DHIDI YA ZANZIBAR
Kila sifa njema anastahiki Mwenyezi Mungu Mtukufu Mlezi wa Viumbe. Sala na salamu zimfikie Mtume wetu Mtukufu Muhammad (S.A.W), jamaa zake, maswahaba zake waongofu na wote wanaowafuata kwa wema hadi Siku ya Malipo.
Baraza la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Zanzibar lililokaa Jumapili tarehe 23/2/2013 katika kikao cha kutathmini matukio ya kushambuliwa na kuuliwa viongozi wa Dini yakiwemo ya karibuni ya kupigwa risasi na kuuliwa Padri Mushi pamoja na kupigwa mapanga na kuuliwa Sheikh Ali Khamis Bin Ali Khatibu wa Mwakaje na kuendelea kutolewa kwa kauli za uchochezi dhidi ya Zanzibar linatamka ifuatavyo:
1. Baraza la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Zanzibar linalaani vikali na kwa nguvu zote matukio ya kushambuliwa na kuuliwa viongozi wa Dini likiwemo tukio la karibuni la kupigwa risasi na kuuwawa Padri Mushi kulikofanywa na wahalifu wasioitakia mema Zanzibar.

2. Baraza la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Zanzibar linapenda kuweka wazi kuwa uhai ni tunu kubwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu aliyotunukiwa binaadamu hivyo hakuna mwenye mamlaka ya kuiondoa haki hiyo isipokuwa yeye mweyewe Mwenyezi Mungu. Kutokana na ukweli huu ndio maana Sheria za Kiislamu zimeweka wazi mtu mwenye kumuuwa mwenziwe naye auliwe kama inavyoelezwa katika Kitabu kitufu cha Quran kama ifuatavyo:

“Na humo (katika Taurati) tuliwaandikia ya kwamba mtu (huuwawa kwa sababu ya kuuwa mtu) kwa mtu, ……….” (5:44)

Hivyo, vitendo vya kiharamia vya kushambuliwa viongozi wa Dini kulikoanzia kwa kumwagiwa tindi kali Sheikh Soraga, kupigwa risasi Padri Ambrose Mkenda, kuuliwa Padri huko Musoma, kupigwa risasi na kuuwawa Padri Mushi na kushambuliwa kwa mapanga na kuuliwa Sheikh Ali Khamis Bin Ali Khatibu wa Mwakaje kwa dhulma kulikofanywa na wahalifu ni jambo lisilokubalika na Uislamu na Waislamu wenyewe. Aidha wahusika wa matendo haya wawe wafuasi wa Dini yoyote ile bado watahesabika ni wahalifu kwani vitendo vya kihalifu na kiharamia kamwe haviwezi kunasibishwa na Dini fulani.
3. Baraza la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Zanzibar linaviomba vyombo husika kufanya upelelezi wa kina kuhusu matukio haya kwa kuzingatia uadilifu na misingi ya kazi zao ili kuwabaini wahalifu na kufikishwa katika vyombo vya kisheria. Aidha Baraza linavitahadharisha vyombo hivyo kuepuka kufanya kazi yao kwa kusukumwa na matashi binafsi, jazba, chuki, matashi ya baadhi ya wanasiasa na viongozi wa Dini pamoja na shindikizo la baadhi ya vyombo vya habari.
4. Baraza la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Zanzibar linalaani na kupinga kwa nguvu zake zote kauli aliyoitoa Waziri wa Mambo ya Ndani wa Tanzania na baadhi ya vyombo vya habari kuihusisha Zanzibar na ugaidi kutokana na tukio la kuuliwa Padri Mushi. Kauli hii inaonesha kuwa Mheshimiwa Waziri anaibagua Zanzibar katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwasababu tunavyoelewa sisi suala la usalama wa nchi ni suala la Muungano hivyo huwezi kuihusisha Zanzibar pekee na suala la ugaidi. Hivyo, Baraza linaona kuwa kauli hizi zinazotolewa ni mbinu za makusudi za kuichafua Zanzibar katika Jumuiya ya Kimataifa kutokana na chuki binafsi dhidi ya Zanzibar na watu wake.
5. Aidha Baraza la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Zanzibar linamtaka Mheshimiwa Waziri kwa kulinda heshima yake kuwajibika kwa Watanzania kwa kujiuzulu kutokana na kushindwa kulinda usalama wa wananchi wakiwemo viongozi wa Dini ambao ndio walezi wa jamii.
6. Baraza la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Zanzibar linalaani kauli za uchochezi zinazoendelea kutolewa na baadhi ya vyombo vya habari zinazochochea chuki, uadui, hasama na mtafaruku kati ya Waislamu na Wakristo na kusahau kuwa Waislamu wameishi na Wakristo kwa amani, mapenzi na mashirikiano hapa Zanzibar karne na karne. Baraza linaona kuwa vyombo hivyo vya habari vinatekeleza ajenda ya kuivuruga Zanzibar kwa kuchochea vita vya kidini ili kufikia malengo yao wanayoyajua wenyewe. Hivyo, Baraza linaiomba Serikali kuvidhibiti kwa kuvichukulia hatua vyombo vyote vinavyotumia matukio haya kuchochea uadui na chuki kati ya Waislamu na Wakristo.
7. Baraza la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Zanzibar linaviomba vyombo vya habari vya Zanzibar kuwajibika kwa Wazanzibari wanaolipa kodi kwa kuwapasha taarifa sahihi juu ya matukio muhimu yanayotokea katika jamii yao badala ya wananchi kutegemea kupokea taarifa za upotoshaji na uchochezi kutoka katika vyombo vya habari visivyotutakia mema.
8. Baraza la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Zanzibar linaziomba Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Zanzibar kuwasilisha kwa Watanzania taarifa ya wazi ya matokeo ya uchunguzi wa matukio haya kwa kuanzia na lile la kumwagiwa tindi kali Sheikh Soraga, kupigwa risasi Padri Ambrose Mkenda, kuuliwa Padri huko Musoma, kupigwa risasi na kuuwawa Padri Mushi na kushambuliwa kwa mapanga na kuuliwa Sheikh Ali Khamis Bin Ali Khatibu wa Mwakaje.
9. Baraza la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Zanzibar linawaomba Wazanzibari wote kuwa watulivu katika kipindi hichi ambapo upelelezi wa matukio haya ukiendelea. Aidha Baraza linawasihi Wazanzibari wote bila ya kujali tofauti zao za kidini kulinda umoja wao na kudumisha amani pamoja na kukataa kugawanywa ili kuwatoa katika ajenda yao ya msingi ya kudai Mamlaka Kamili ya Zanzibar katika Muungano.

MOLA WETU MTUKUFU TUNAKUOMBA UINUSURU ZANZIBAR NA WATU WAKE DHIDI YA MAADUI WA NDANI NA NJE WASIOITAKIA MEMA NCHI YETU
Imesainiwa na:

Sheikh Ali Abdalla Shamte

Amir wa Baraza la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Zanzibar


Saturday, February 23, 2013

MWENYEZI MUNGU HUPOKEA TOBA ZA WANADAMU USIKU NA MCHANA


Hadiyth Ya 2, Katika kitabu cha Hadithi za Mtume (s.a.w.): LU-ULU-UN MANTHUWRUN 
Allaah Hupokea Tawbah Za Waja Usiku Na Mchana

عَنْ أَبِي مُوسَى عَبْدِ الله بنِ قَبَسٍ الأَشْعَرِيِّ  (رضي الله عنه) عن النَّبيّ (صلى الله عليه و آله وسلم) قال: ((إِنَّ اللَّهَ تَعَالَى يَبْسُطُ يَدَهُ بِاللَّيْلِ لِيَتُوبَ مُسِيءُ النَّهَارِ وَيَبْسُطُ يَدَهُ بِالنَّهَارِ لِيَتُوبَ مُسِيءُ اللَّيْلِ حَتَّى تَطْلُعَ الشَّمْسُ مِنْ مَغْرِبِهَا)) رواه مسلم
Imepokelewa kutoka kwa Abu Muwsaa ‘Abdillaah bin Qays Al-Ash‘ariyy (رضي الله عنه)  kwamba Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Hakika Allaah Anakunjua Mkono Wake usiku ili Apokee tawbah ya mkoseaji mchana. Na Anakunjua Mkono Wake mchana ili Apokee tawbah ya mkoseaji usiku mpaka jua lichomoze Magharibi [mahali linapokuchwa]))[1]

Mafunzo Na Hidaaya:
  1. Umuhimu wa mja kukimbilia kutubu anapofanya maasi mchana au usiku. [At-Tahriym 66: 8, An-Nuwr 24: 31].
وَسَارِعُوا إِلَىٰ مَغْفِرَةٍ مِّن رَّبِّكُمْ وَجَنَّةٍ عَرْضُهَا السَّمَاوَاتُ وَالْأَرْضُ أُعِدَّتْ لِلْمُتَّقِينَ
Na kimbilieni maghfirah kutoka kwa Mola wenu na Jannah upana wake ni wa mbingu na ardhi imeandaliwa kwa wenye taqwa[2]
  1. Rahma ya Allaah (سبحانه وتعالى) kwa waja Wake kuwapa muda wa kutubia maasi, lau sivyo Angeliwaadhibu na kuwaangamiza hapo hapo wanapotenda maasi. [Faatwir 35: 45, An-Nahl 16: 61].
  1. Rahma ya Allaah kwa waja Wake kutokutofautisha wakati wa tawbah japokuwa maasi mengine yanazidi mengineyo. 
  1.  Tawbah inaendelea kupokelewa hadi milango ifungwe: [Hadiyth: ((Hakika Allaah Huikubali tawbah ya mja Wake kabla ya roho kufika kwenye mkoromo wa mauti))[3] ((Atakayetubu kabla ya kuchomoza jua upande wa Magharibi, Allaah Atamkubalia tawbah yake)).[4]
  1. Hii inaonyesha mahaba makubwa ya Allaah (سبحانه وتعالى) kwa kuwapatia fursa hii ya dhahabu ambayo haifai kupotezwa na waja wenyewe.
  1. Hadiyth inatoa mafunzo kwa Muislamu kutokumhukumu mwenziwe kuwa hatoghufuriwa madhambi yake. [Rejea Hadiyth namba 99].
  1. Mja hata afanye madhambi makubwa vipi, asikate tamaa na Rahma ya Allaah (سبحانه وتعالى), kwani Yeye Hughufuria madhambi yote. [Az-Zumar 39: 53]



[1]  Muslim.
[2]  Aal-‘Imraan (3: 133).
[3]  At-Tirmidhiy, Ibn Maajah, Ahmad, na imepewa daraja ya Swahiyh na Al-Albaaniy.
[4]  Muslim.

Wednesday, February 20, 2013

PICHA KATIKA MAZISHI YA PADRE ALIYEUAWA KWA RISASI ZANZIBAR


  Wanafunzi wa skuli ya Kikristu wakihudhuria ibada ya Mazishi ya Mchungaji Evaristus.G.Mushi iliofanyika katika Kanisa la Minara Miwili liliopo Shangani Mjini Zanzibar,Mchungaji alifariki Dunia Baada ya Kupigwa Risasi na Watu wasiojulikana huko Beitrasi Mjini Zanzibar.



    Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohd Shein akisalimiana na Askofu wa Kanisa katoliki Zanzibar Augustino Shao mara alipowasili katika Kanisa la Minara Miwili liliopo Shangani Mjini Zanzibar ili kuuwaga Mwili wa Marehemu Mchungaji Evaristus.G.Mushi aliefariki kwa kupigwa Risasi na watu wasiojulikana huko Beitrasi Mjini Zanzibar.




   Waumini wa Madhebu mbalimbali wakimiminika katika Kanisa la Minara Miwili liliopo Shangani Mjini Zanzibar ili kuuwaga Mwili wa Marehemu Mchungaji Evaristus.G.Mushi aliefariki kwa kupigwa Risasi na watu wasiojulikana huko Beitrasi Mjini Zanzibar.




Jeneza lililobeba Mwili wa Marehemu Mchungaji Evaristus.G.Mushi likipelekwa katika kaburi kwa ajili ya mazishi ambayo yalifanyika huko katika kijiji cha Kitope wilaya ya Kaskazini B Zanzibar.   

    Mazishi ya Mchungaji Evarist Mushi yamefanyika leo tarehe   
     20/02/2013 Zanzibar.
  
    Picha na Zanzibar Daima Blog.