Wednesday, February 20, 2013

PICHA KATIKA MAZISHI YA PADRE ALIYEUAWA KWA RISASI ZANZIBAR


  Wanafunzi wa skuli ya Kikristu wakihudhuria ibada ya Mazishi ya Mchungaji Evaristus.G.Mushi iliofanyika katika Kanisa la Minara Miwili liliopo Shangani Mjini Zanzibar,Mchungaji alifariki Dunia Baada ya Kupigwa Risasi na Watu wasiojulikana huko Beitrasi Mjini Zanzibar.



    Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohd Shein akisalimiana na Askofu wa Kanisa katoliki Zanzibar Augustino Shao mara alipowasili katika Kanisa la Minara Miwili liliopo Shangani Mjini Zanzibar ili kuuwaga Mwili wa Marehemu Mchungaji Evaristus.G.Mushi aliefariki kwa kupigwa Risasi na watu wasiojulikana huko Beitrasi Mjini Zanzibar.




   Waumini wa Madhebu mbalimbali wakimiminika katika Kanisa la Minara Miwili liliopo Shangani Mjini Zanzibar ili kuuwaga Mwili wa Marehemu Mchungaji Evaristus.G.Mushi aliefariki kwa kupigwa Risasi na watu wasiojulikana huko Beitrasi Mjini Zanzibar.




Jeneza lililobeba Mwili wa Marehemu Mchungaji Evaristus.G.Mushi likipelekwa katika kaburi kwa ajili ya mazishi ambayo yalifanyika huko katika kijiji cha Kitope wilaya ya Kaskazini B Zanzibar.   

    Mazishi ya Mchungaji Evarist Mushi yamefanyika leo tarehe   
     20/02/2013 Zanzibar.
  
    Picha na Zanzibar Daima Blog.




No comments: