Sunday, February 17, 2013

PADRI EVARIST MUSHI AUAWA ZANZIBAR

 Ni Padri Mushi ambaye alikuwa ni Paroko wa Parokia ya Minara Miwili – Zanzibar
Amepigwa risasi na watu wasiojulikana leo mida ya saa moja asubuhi akielekea kanisani
Taarifa zilizopatikana sasa hivi ni kuwa Paroko wa Kanisa la Katoliki Minara Miwili Zanzibar, Evarist Mushi amefariki dunia baada ya kupigwa risasi saa 1.00 asubuhi na kufariki kabla hajafika hospitali ya Mnazi Mmoja. Paroko huyu amepigwa risasi akishuka katika gari lake wakati akienda kuendesha ibada ya saa 3.00 leo.
Padri Evarist Mushi amepigwa risasi kichwani na kufa papohapo na watu wasiojulikana akiwa njiani anaenda kuendesha misa katika Kanisa la Mt.Theresia eneo la Mtoni Zanzibar.
Msemaji wa Polisi Zanzibar, Inspekta Mohamed Mhina amethibitisha tokeo hilo.
SOURCES: Mzalendo.net, zanzibaryetu.wordpress.com na blogs mbalimbali za Kitanzania

No comments: