Monday, September 28, 2015

ASILI YA ROHO (NAFSI) ZETU

Kuna umuhimu mkubwa wa kuzungumzia kuhusu roho (nafsi) zetu ambazo zinahitaji kutoharishwa  ili ziwe  katika hali   ya asili yake, (kama zilivyokuwa kabla ya kupulizwa katika mwili wa binaadamu)   na ambazo ndio zitakuwa sababu ya kufaulu  au kufeli kwetu duniani na akhera.  
((وَيَسْأَلُونَكَ عَنِ الرُّوحِ قُلِ الرُّوحُ مِنْ أَمْرِ رَبِّي وَمَا أُوتِيتُم مِّن الْعِلْمِ إِلاَّ قَلِيلاً))
((Na wanakuuliza (ewe Muhammad)  khabari za Roho. Sema: Roho ni katika mambo ya Mola wangu Mlezi. Nanyi hamkupewa katika ilimu ila kidogo tu))   [Al-Israa::85]