Tuesday, October 22, 2013

Nimemdanganya Mume Wangu, Je, Nimeachika? Na Je, Inanipasa Nikae Eda


SWALI:
Bibi na Bwana wameelewana kutumia koil kukinga kupata mtoto kwa mda. Kisha bwana ameamua koil bibi akaitowe. Bibi akamwambia bwana haya. Ikapita mdaa. Bwana akamuuliza bibi kama ile koil ameitoa? Bibi akadaganya mumewe kwamba koil kesha itowa. Baadae siku kadha bwana akamwambia bibi nafikiri kua koil hujaitoa umenidaganya. Na kama umenidaganya jua nishakuwacha. Bibi ana watoto watatu. WA miaka mitatu, na miwili na mmoja. Kazi ya ulezi pekee yake. Sababu bwana anafanya kazi kuazia jumatatu hadi ijumaa.   Swala langu ni, jee huyu mwanake kishawachika? Swala la pili kwa kua anahakika kua anatumia koil kutokupata mimba jee. Jee akiachika anakaa edaa? Insha’Allah nitapata majibu ya kuniridhisha. Asalaam aleikum.

Wednesday, August 21, 2013

NAFASI ZA KAZI KATIKA TAASISI YA UTAFITI WA MIFUGO (TALIRI) NALIENDELE - MTWARA


THE UNITED REPULIC OF TANZANIA
MINISTRY OF LIVESTOCK AND FISHERIES DEVELOPMENT

Telegrams: Scientific Mtwara                                   Tanzania Livestock Research Institute
Tel: +255 073 293 4035                                         Naliendele
Fax: +255 073 293 41                                            P. O. Box 509
Email: utafiti@iwayafrica.com                                  MTWARA
            In reply please quote:
            Kumb Na. MLD/NAL/F/2/Vol. 1/38

KWA YEYOTE ANYEHUSIKA:

YAH: NAFASI ZA KAZI KATIKA TAASISI YA UTAFITI WA MIFUGO (TALIRI) NALIENDELE-MTWARA

Tafadhali rejeeni kichwa cha habari hapo juu.

Napenda kuwatangazia kuwa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) iliyoanzishwa kwa Sheria Namba 4. Ya mwaka 2012 ya bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inazo nafasi za kazi kwa wale watakaopenda kufanya kazi katika Taasisi ua Utafiti wa Mifugo Naliendele-Mtwara. Nafasi zilizopo kwa sasa ni kama ifuatavyo:

Wednesday, August 7, 2013

MAMBO MATATU YANAYOFUATIA RAMADHAN


Zakaatul-Fitwr, 'Iydul-Fitwr Na Swawm Ya Sittatush Shawwaal

Tunakaribia kumaliza mwezi Mtukufu wa Ramadhaan na mambo matatu yafuatayo ya muhimu yanayotukabili yanapasa kuzingatiwa ili tukamilishe Swawm zetu ipasavyo na tupate fadhila zake.

1- ZAKAATUL-FITWR  
Inaitwa Zakaatul-Fitwr (Zakaah ya Kufuturu au Kufutari) kutokana na kumalizika Swawm ya Ramadhaan. Imefaridhiwa mwaka wa pili wa Hijrah katika mwezi wa Ramadhaan. 
Hikmah Yake
Ni kutwaharisha Swawm ya Muislamu kutokana na maneno machafu, ya upuuzi wakati alipokuwa amefunga kwa kulisha maskini chakula ili nao wapate chakula kizuri siku ya ‘Iyd.

Friday, August 2, 2013

ZAKAATUL FITWR


Zakaah Apewe Nani? 
SWALI
Zakaatul-Fitwr apewe nani? Je, inaruhusiwa kuituma mfano kwa Mujaahidiyn waliko vitani? Au kuitoa katika vyama vinavyokusanya sadaka au kujengea msikiti?

JIBU:
Sifa zote ni za Allaah.
Zakaatul-Fitwr inapaswa kupewa maskini Waislamu katika nchi au mji ambao inatolewa kwa sababu ya usimulizi wa Abu Daawuud kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhiya Allaahu 'anhuma) ambaye amesema: "Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ameamrisha Zakaatul-Fitwr ilipwe Ramadhaan kuwalisha watu masikini…."

Inaruhusiwa kuituma kwa masikini wa nchi nyingine ambao watu wake wanahitaji zaidi. Hairuhusiwi kujengea msikiti au kuitoa katika miradi ya sadaka.
Halmashauri ya Kudumu ya Utafiti Wa Kiislaam na utoaji wa Fatwa.

Tuesday, July 30, 2013

MASIKU YA KUMI LA MWISHO LA MWEZI WA RAMADHAN


Masiku ya kumi la mwisho la mwezi mtukufu wa Ramadhani, yana fadhila na khususia nyingi kathiri, miongoni mwake ni pamoja na kwamba:
i. Ndani ya masiku hayo umo usiku wa cheo/heshima, ambao huo ni bora kuliko miezi alfu moja. Na ye yote atakaye simama kufanya ibada katika usiku huo, kwa kumuamini Allah kikweli na kwa kutaraji ujira kutoka kwake, huyo atasamehewa dhambi alizokwisha zitenda.

Saturday, July 6, 2013

MWEZI WA RAMADHAAN IMETEREMSHWA QUR-AAN - JICHUMIE FADHILA ZA KUSOMA NA KUHIFADHI QUR-AAN

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala)  
(( شَهْرُ رَمَضَانَ الَّذِيَ أُنزِلَ فِيهِ الْقُرْآنُ هُدًى لِّلنَّاسِ وَبَيِّنَاتٍ مِّنَ الْهُدَى وَالْفُرْقَانِ))

((Mwezi wa Ramadhaan ambao imeteremshwa humo Qur-aan kuwa ni uongofu kwa watu, na hoja zilizo wazi za uongofu na upambanuzi)) [Al-Baqarah: 184]
Kwa hivyo basi ndugu Muislamu, jitahidi ufanye ibada hii adhimu usome na kuhifadhi Qur-aan kwa wingi kabisa kwani thawabu na fadhila zake ni nyingi na adhimu mno kama tunavyozinukuu humu. Pia jitahidi uweze kuhitimisha (kumaliza kuisoma) japo mara moja Qur-aan nzima kabla ya mwezi wa Ramadhaan kwisha.

Tuesday, June 25, 2013

NJIA10 ZA KUUKARIBISHA VIZURI MWEZI WA RAMADHAN

Anasema Allaah سبحانه وتعالى:

((يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُواْ كُتِبَ عَلَيْكُمُ الصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ)) (( أَيَّامًا مَّعْدُودَاتٍ فَمَن كَانَ مِنكُم مَّرِيضًا أَوْ عَلَى سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ وَعَلَى الَّذِينَ يُطِيقُونَهُ فِدْيَةٌ طَعَامُ مِسْكِينٍ فَمَن تَطَوَّعَ خَيْرًا فَهُوَ خَيْرٌ لَّهُ وَأَن تَصُومُواْ خَيْرٌ لَّكُمْ إِن كُنتُمْ تَعْلَمُونَ))  ((شَهْرُ رَمَضَانَ الَّذِيَ أُنزِلَ فِيهِ الْقُرْآنُ هُدًى لِّلنَّاسِ وَبَيِّنَاتٍ مِّنَ الْهُدَى وَالْفُرْقَانِ فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ وَمَن كَانَ مَرِيضًا أَوْ عَلَى سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ يُرِيدُ اللّهُ بِكُمُ الْيُسْرَ وَلاَ يُرِيدُ بِكُمُ الْعُسْرَ وَلِتُكْمِلُواْ الْعِدَّةَ  وَلِتُكَبِّرُواْ اللّهَ عَلَى مَا هَدَاكُمْ  وَلَعَلَّكُمْ  تَشْكُرُونَ))  
((Enyi mlioamini! Mmefaradhishiwa Swawm, kama waliyofaradhishiwa waliokuwa kabla yenu ili mpate kumcha Allaah))(([Mfunge] siku maalumu za kuhisabika. Na atakayekuwa miongoni mwenu mgonjwa au yumo safarini basi atimize hisabu katika siku nyengine. Na wale wasioweza, watoe fidiya kwa kumlisha masikini. Na atakayefanya wema kwa kujitolea, basi ni bora kwake. Na mkifunga ni bora kwenu, kama mnajua))  ((Mwezi wa Ramadhaan ambao imeteremshwa humo Qur-aan kuwa ni uongofu kwa watu, na hoja zilizo wazi za uongofu na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini katika mwezi huu na afunge. Na mwenye kuwa mgonjwa au safarini, basi atimize hisabu katika siku nyengine. Allaah Anakutakieni yaliyo mepesi wala Hakutakieni yaliyo mazito, na mtimize hiyo hisabu, na mumtukuze Allaah  kwa kuwa Amekuongoeni ili mpate kushukuru)) [Al-Baqarah: 183-185]