Sunday, November 3, 2013

MATOKEO YA DARASA LA SABA 2013, HAYA HAPA

 
 
Matokeo ya Darasa la Saba yametangazwa jana na mwaka huu ufaulu umeongezeka kutoka asilimia 30.72 mwaka jana mbaka asilimia 50.61 mwaka huu kutokana na wanafunzi walio fanya mtihani mwaka huu wa darasa la saba kufaulu zaidi ukilinganisha na wanafunzi wa mwaka jana.
Kaimu mtendaji wa Baraza la Mtihani Charles Msonda amesema ufaulu katika masomo yote umepanda kwa asilimia kati ya 6.01 na 28.06 ukilinganisha na mwaka 2012 Mwaka huu watahiniwa wamefaulu zaidi katika somo la Kiswahili kwa asilimia 69.06 na somo walio faulu kwa kiwango kidogo zaidi ni somo la Hisabati wamefaulu kwa asilimia 28.62, Msonda amesema jumla ya watahiniwa 427,606 kati ya 844,938 walio fanya mtihani huo wamepata alama ya 100 kati ya alama ya 250 idadi hiyo ni sawa na asilimia 50.61.
 

Saturday, November 2, 2013

Du’aa Ya Malaika Kila Siku Kwa Mtoaji Sadaka Na Mzuiaji

 عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه)  أَنَّ النَّبِيَّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((مَا مِنْ يَوْمٍ يُصْبِحُ الْعِبَادُ فِيهِ إلاَّ مَلَكَانِ يَنْزِلاَنِ فَيَقُولُ أَحَدُهُمَا: اللَّهُمَّ أَعْطِ مُنْفِقًا خَلَفًا. وَيَقُولُ الأَخَرُ: اللَّهُمَّ أَعْطِ مُمْسِكًا تَلَفًا)) متفق عليه
Imepokelewa kutoka kwa Abu Hurayrah(رضي الله عنه)  kwamba Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Kila siku inayowapambaukia watu kuna Malaika wawili wanateremka, mmoja wao akiomba: Ee Allaah! Mwenye kutoa [sadaka] mlipe zaidi. Na mwengine huomba: Ee Allaah! Mwenye kuzuia mpe hasara)).[1]

Sunday, October 27, 2013

Mwanamke Asifunge Swawm Au Kumuingiza Mtu Kwenye Nyumba Bila Ya Idhini Ya Mumewe

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه)  أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((لاَ يَحِلُّ لِلْمَرْأَةِ أَنْ تَصُومَ وَزَوْجُهَا شَاهِدٌ إلاَّ بِإِذْنِهِ. وَلاَ تَأْذَنَ فِي بَيْتِهِ إلاَّ بِإِذْنِهِ)) متفق عليه وهذا لفظ البخاري
Imepokelewa kutoka kwa Abu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Mtume wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Si halali kwa mwanamke kufunga Swawm [ya Sunnah] ilhali mumewe yupo [hakusafiri] ila kwa idhini yake. Wala asimruhusu mtu kuingia nyumbani kwake ila kwa idhini yake)).[1]
 

Tuesday, October 22, 2013

Nimemdanganya Mume Wangu, Je, Nimeachika? Na Je, Inanipasa Nikae Eda


SWALI:
Bibi na Bwana wameelewana kutumia koil kukinga kupata mtoto kwa mda. Kisha bwana ameamua koil bibi akaitowe. Bibi akamwambia bwana haya. Ikapita mdaa. Bwana akamuuliza bibi kama ile koil ameitoa? Bibi akadaganya mumewe kwamba koil kesha itowa. Baadae siku kadha bwana akamwambia bibi nafikiri kua koil hujaitoa umenidaganya. Na kama umenidaganya jua nishakuwacha. Bibi ana watoto watatu. WA miaka mitatu, na miwili na mmoja. Kazi ya ulezi pekee yake. Sababu bwana anafanya kazi kuazia jumatatu hadi ijumaa.   Swala langu ni, jee huyu mwanake kishawachika? Swala la pili kwa kua anahakika kua anatumia koil kutokupata mimba jee. Jee akiachika anakaa edaa? Insha’Allah nitapata majibu ya kuniridhisha. Asalaam aleikum.

Wednesday, August 21, 2013

NAFASI ZA KAZI KATIKA TAASISI YA UTAFITI WA MIFUGO (TALIRI) NALIENDELE - MTWARA


THE UNITED REPULIC OF TANZANIA
MINISTRY OF LIVESTOCK AND FISHERIES DEVELOPMENT

Telegrams: Scientific Mtwara                                   Tanzania Livestock Research Institute
Tel: +255 073 293 4035                                         Naliendele
Fax: +255 073 293 41                                            P. O. Box 509
Email: utafiti@iwayafrica.com                                  MTWARA
            In reply please quote:
            Kumb Na. MLD/NAL/F/2/Vol. 1/38

KWA YEYOTE ANYEHUSIKA:

YAH: NAFASI ZA KAZI KATIKA TAASISI YA UTAFITI WA MIFUGO (TALIRI) NALIENDELE-MTWARA

Tafadhali rejeeni kichwa cha habari hapo juu.

Napenda kuwatangazia kuwa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) iliyoanzishwa kwa Sheria Namba 4. Ya mwaka 2012 ya bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inazo nafasi za kazi kwa wale watakaopenda kufanya kazi katika Taasisi ua Utafiti wa Mifugo Naliendele-Mtwara. Nafasi zilizopo kwa sasa ni kama ifuatavyo:

Wednesday, August 7, 2013

MAMBO MATATU YANAYOFUATIA RAMADHAN


Zakaatul-Fitwr, 'Iydul-Fitwr Na Swawm Ya Sittatush Shawwaal

Tunakaribia kumaliza mwezi Mtukufu wa Ramadhaan na mambo matatu yafuatayo ya muhimu yanayotukabili yanapasa kuzingatiwa ili tukamilishe Swawm zetu ipasavyo na tupate fadhila zake.

1- ZAKAATUL-FITWR  
Inaitwa Zakaatul-Fitwr (Zakaah ya Kufuturu au Kufutari) kutokana na kumalizika Swawm ya Ramadhaan. Imefaridhiwa mwaka wa pili wa Hijrah katika mwezi wa Ramadhaan. 
Hikmah Yake
Ni kutwaharisha Swawm ya Muislamu kutokana na maneno machafu, ya upuuzi wakati alipokuwa amefunga kwa kulisha maskini chakula ili nao wapate chakula kizuri siku ya ‘Iyd.

Friday, August 2, 2013

ZAKAATUL FITWR


Zakaah Apewe Nani? 
SWALI
Zakaatul-Fitwr apewe nani? Je, inaruhusiwa kuituma mfano kwa Mujaahidiyn waliko vitani? Au kuitoa katika vyama vinavyokusanya sadaka au kujengea msikiti?

JIBU:
Sifa zote ni za Allaah.
Zakaatul-Fitwr inapaswa kupewa maskini Waislamu katika nchi au mji ambao inatolewa kwa sababu ya usimulizi wa Abu Daawuud kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhiya Allaahu 'anhuma) ambaye amesema: "Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ameamrisha Zakaatul-Fitwr ilipwe Ramadhaan kuwalisha watu masikini…."

Inaruhusiwa kuituma kwa masikini wa nchi nyingine ambao watu wake wanahitaji zaidi. Hairuhusiwi kujengea msikiti au kuitoa katika miradi ya sadaka.
Halmashauri ya Kudumu ya Utafiti Wa Kiislaam na utoaji wa Fatwa.