Tuesday, July 22, 2014

OVERALL SUMMARY OF RESULTS FOR CGA 2013 SEMESTER II



MINISTRY OF AGRICULTURE FOOD SECURITY AND COOPERATIVES
DEPARTMENTOF TRAINING INSTITUTES
MATI MTWARA
OVERALL SUMMARY OF RESULTS FOR CGA 2013 SEMESTER II
EXAMINATION NO. 111 - 224

OVERALL SUMMARY OF RESULTS FOR CGA 2013 SEMESTER II



MINISTRY OF AGRICULTURE FOOD SECURITY AND COOPERATIVES
DEPARTMENTOF TRAINING INSTITUTES
MATI MTWARA
OVERALL SUMMARY OF RESULTS FOR CGA 2013 SEMESTER II
EXAMINATION NI. 1 - 110

OVERALL SUMMARY OF RESULTS FOR DGA 2013 SEMESTER II



MINISTRY OF AGRICULTURE FOOD SECURITY AND COOPERATIVES
DEPARTMENTOF TRAINING INSTITUTES
MATI MTWARA
OVERALL SUMMARY OF RESULTS FOR DGA 2013 SEMESTER II

Sunday, July 20, 2014

USIKU WA CHEO (LAYLATUL QADR)



Laylatul-Qadr- Vipi Uweze Kuupata Usiku Huu?
Tunakaribia kuingia kumi la mwisho, kumi ambalo ndani yake kuna usiku unaojulikana kama ni: Laylatul-Qadr. Ibaada yoyote itakayotendwa usiku huo, ni bora kuliko ibaada ya miezi elfu.
Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):   
 بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ. إِنَّا أَنزَلْنَاهُ فِي لَيْلَةِ الْقَدْرِ ﴿١﴾ وَمَا أَدْرَاكَ مَا لَيْلَةُ الْقَدْرِ ﴿٢﴾ لَيْلَةُ الْقَدْرِ خَيْرٌ مِّنْ أَلْفِ شَهْرٍ ﴿٣﴾ تَنَزَّلُ الْمَلَائِكَةُ وَالرُّوحُ فِيهَا بِإِذْنِ رَبِّهِم مِّن كُلِّ أَمْرٍ ﴿٤﴾ سَلَامٌ هِيَ حَتَّىٰ مَطْلَعِ الْفَجْرِ ﴿٥﴾
BismiLLaahir-Rahmaanir-Rahiym (Kwa Jina la Allaah Mwingi wa Rehma, Mwenye kurehemu). Hakika Sisi Tumeiteremsha (Qur-aan) katika Laylatil-Qadr (usiku wa cheo). Na nini kitakachokujulisha ni nini huo (usiku wa) Laylatul-Qadr? (Usiku wa) Laylatul-Qadr ni (usiku) mbora kuliko miezi elfu. Wanateremka humo Malaika na Ruwh (Jibriyl) kwa idhini ya Mola wao kwa kila amri (jambo). (Usiku huo ni) Amani mpaka kuchomoza Alfajiri   (Al-Qadr: 1-5)

Sunday, January 5, 2014

SIFA NNE ZA KUCHAGUA MKE MWEMA


Sifa Nne Za Kuchagua Mke: Mali, Nasaba, Uzuri Na Dini

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((تُنْكَحُ الْمَرْأَةُ لأَرْبَعٍ: لِمَالِهَا, وَلِحَسَبِهَا, وَجَمَالِهَا, وَلِدِينِهَا. فَاظْفَرْ بِذَاتِ الدِّينِ تَرِبَتْ يَدَاكَ)) متفق عليه

Imepokelewa kutoka kwa Abu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Mwanamke huolewa kwa sababu nne; Kwa mali yake, nasaba yake [ukoo], uzuri wake na Dini yake. Tafuta mwenye Dini uwe salama)).[1]  (yaani usiharibikiwe katika maisha yako)

 Mafunzo Na Hidaaya:
  1. Uislamu umetoa uongofu katika kila jambo hata katika kutafuta mke mwema. 

Sunday, November 3, 2013

MATOKEO YA DARASA LA SABA 2013, HAYA HAPA

 
 
Matokeo ya Darasa la Saba yametangazwa jana na mwaka huu ufaulu umeongezeka kutoka asilimia 30.72 mwaka jana mbaka asilimia 50.61 mwaka huu kutokana na wanafunzi walio fanya mtihani mwaka huu wa darasa la saba kufaulu zaidi ukilinganisha na wanafunzi wa mwaka jana.
Kaimu mtendaji wa Baraza la Mtihani Charles Msonda amesema ufaulu katika masomo yote umepanda kwa asilimia kati ya 6.01 na 28.06 ukilinganisha na mwaka 2012 Mwaka huu watahiniwa wamefaulu zaidi katika somo la Kiswahili kwa asilimia 69.06 na somo walio faulu kwa kiwango kidogo zaidi ni somo la Hisabati wamefaulu kwa asilimia 28.62, Msonda amesema jumla ya watahiniwa 427,606 kati ya 844,938 walio fanya mtihani huo wamepata alama ya 100 kati ya alama ya 250 idadi hiyo ni sawa na asilimia 50.61.
 

Saturday, November 2, 2013

Du’aa Ya Malaika Kila Siku Kwa Mtoaji Sadaka Na Mzuiaji

 عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه)  أَنَّ النَّبِيَّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((مَا مِنْ يَوْمٍ يُصْبِحُ الْعِبَادُ فِيهِ إلاَّ مَلَكَانِ يَنْزِلاَنِ فَيَقُولُ أَحَدُهُمَا: اللَّهُمَّ أَعْطِ مُنْفِقًا خَلَفًا. وَيَقُولُ الأَخَرُ: اللَّهُمَّ أَعْطِ مُمْسِكًا تَلَفًا)) متفق عليه
Imepokelewa kutoka kwa Abu Hurayrah(رضي الله عنه)  kwamba Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Kila siku inayowapambaukia watu kuna Malaika wawili wanateremka, mmoja wao akiomba: Ee Allaah! Mwenye kutoa [sadaka] mlipe zaidi. Na mwengine huomba: Ee Allaah! Mwenye kuzuia mpe hasara)).[1]