Tuesday, July 30, 2013

MASIKU YA KUMI LA MWISHO LA MWEZI WA RAMADHAN


Masiku ya kumi la mwisho la mwezi mtukufu wa Ramadhani, yana fadhila na khususia nyingi kathiri, miongoni mwake ni pamoja na kwamba:
i. Ndani ya masiku hayo umo usiku wa cheo/heshima, ambao huo ni bora kuliko miezi alfu moja. Na ye yote atakaye simama kufanya ibada katika usiku huo, kwa kumuamini Allah kikweli na kwa kutaraji ujira kutoka kwake, huyo atasamehewa dhambi alizokwisha zitenda.

Saturday, July 6, 2013

MWEZI WA RAMADHAAN IMETEREMSHWA QUR-AAN - JICHUMIE FADHILA ZA KUSOMA NA KUHIFADHI QUR-AAN

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala)  
(( شَهْرُ رَمَضَانَ الَّذِيَ أُنزِلَ فِيهِ الْقُرْآنُ هُدًى لِّلنَّاسِ وَبَيِّنَاتٍ مِّنَ الْهُدَى وَالْفُرْقَانِ))

((Mwezi wa Ramadhaan ambao imeteremshwa humo Qur-aan kuwa ni uongofu kwa watu, na hoja zilizo wazi za uongofu na upambanuzi)) [Al-Baqarah: 184]
Kwa hivyo basi ndugu Muislamu, jitahidi ufanye ibada hii adhimu usome na kuhifadhi Qur-aan kwa wingi kabisa kwani thawabu na fadhila zake ni nyingi na adhimu mno kama tunavyozinukuu humu. Pia jitahidi uweze kuhitimisha (kumaliza kuisoma) japo mara moja Qur-aan nzima kabla ya mwezi wa Ramadhaan kwisha.

Tuesday, June 25, 2013

NJIA10 ZA KUUKARIBISHA VIZURI MWEZI WA RAMADHAN

Anasema Allaah سبحانه وتعالى:

((يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُواْ كُتِبَ عَلَيْكُمُ الصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ)) (( أَيَّامًا مَّعْدُودَاتٍ فَمَن كَانَ مِنكُم مَّرِيضًا أَوْ عَلَى سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ وَعَلَى الَّذِينَ يُطِيقُونَهُ فِدْيَةٌ طَعَامُ مِسْكِينٍ فَمَن تَطَوَّعَ خَيْرًا فَهُوَ خَيْرٌ لَّهُ وَأَن تَصُومُواْ خَيْرٌ لَّكُمْ إِن كُنتُمْ تَعْلَمُونَ))  ((شَهْرُ رَمَضَانَ الَّذِيَ أُنزِلَ فِيهِ الْقُرْآنُ هُدًى لِّلنَّاسِ وَبَيِّنَاتٍ مِّنَ الْهُدَى وَالْفُرْقَانِ فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ وَمَن كَانَ مَرِيضًا أَوْ عَلَى سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ يُرِيدُ اللّهُ بِكُمُ الْيُسْرَ وَلاَ يُرِيدُ بِكُمُ الْعُسْرَ وَلِتُكْمِلُواْ الْعِدَّةَ  وَلِتُكَبِّرُواْ اللّهَ عَلَى مَا هَدَاكُمْ  وَلَعَلَّكُمْ  تَشْكُرُونَ))  
((Enyi mlioamini! Mmefaradhishiwa Swawm, kama waliyofaradhishiwa waliokuwa kabla yenu ili mpate kumcha Allaah))(([Mfunge] siku maalumu za kuhisabika. Na atakayekuwa miongoni mwenu mgonjwa au yumo safarini basi atimize hisabu katika siku nyengine. Na wale wasioweza, watoe fidiya kwa kumlisha masikini. Na atakayefanya wema kwa kujitolea, basi ni bora kwake. Na mkifunga ni bora kwenu, kama mnajua))  ((Mwezi wa Ramadhaan ambao imeteremshwa humo Qur-aan kuwa ni uongofu kwa watu, na hoja zilizo wazi za uongofu na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini katika mwezi huu na afunge. Na mwenye kuwa mgonjwa au safarini, basi atimize hisabu katika siku nyengine. Allaah Anakutakieni yaliyo mepesi wala Hakutakieni yaliyo mazito, na mtimize hiyo hisabu, na mumtukuze Allaah  kwa kuwa Amekuongoeni ili mpate kushukuru)) [Al-Baqarah: 183-185]

Friday, May 10, 2013

TANGAZO KUHUSU NAFASI ZA MAFUNZO YA KILIMO NGAZI YA CHETI NA DIPLOMA KWA MWAKA WA MASOMO 2013/2014



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA KILIMO CHAKULA NA USHIRIKA



TANGAZO KUHUSU NAFASI ZA MAFUNZO YA KILIMO NGAZI YA CHETI NA DIPLOMA KWA MWAKA WA MASOMO 2013/2014
Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika inatangaza nafasi za mafunzo ya Kilimo ngazi ya Cheti na Diploma kwa mwaka wa masomo 2013/14 kama ifuatavyo:

Wednesday, May 1, 2013

HOTUBA YA MH. JAKAYA MRISHO KIKWETE KATIKA SHEREHE YA MAADHIMISHO YA SIKU YA WAFANYAKAZI DUNIANI



Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Nchini (TUCTA),
Ndugu Ayoub Omari Juma;
Mheshimiwa Jaji Mkuu;
Mheshimiwa Gaudensia Kabaka (Mb) Waziri wa Kazi na Ajira;
Mhe. Col Issa Machibya, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro;
Waheshimiwa Mawaziri na Wabunge Mliopo Hapa;
Ndugu Alexio Musindo, Mwakilishi wa Shirika la Kazi Duniani (ILO)


Wednesday, April 17, 2013

NGUZO ZA SWALA, VITENDO VYA WAAJIB NA SUNNAH KATIKA SWALA


بسم الله الرحمن الرحيم


Nguzo za Swalah ni 14: Nguzo ni zile ambazo ukiswali na ukaziacha kwa makusudi Swalah yako inabatilika, na ikiwa umeacha kwa kusahau, Swalah yako pia itakuwa haikukamilika hadi urejee kitendo chenyewe au urejee rakaa na kisha mwishoni utoe Sajdatus-Sahw. Lakini ukiwa umesahau nguzo ya Takbiyratul-Ihraam, basi itakubidi uiswali Swalah upya tokea mwanzo.